Home Makala Yanga sc Vs Usm Algers Fainali Cafcc

Yanga sc Vs Usm Algers Fainali Cafcc

by Sports Leo
0 comments

Mchezo wa fainali ya kombe la shirikisho barani Africa utawajumuisha Yanga sc dhidi ya Usm Algers ya nchini Algeria ambapo timu hizo zimefanikiwa kufuzu katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa ngazi za vilabu barani Afrika.

Yanga sc imefanikiwa kuwaondosha Marumo Gallants ya Afrika ya kusini kwa mabao 4-1 katika michezo miwili ya nyumbani na ugenini huku Usm Algers ikiwatoa Asec Mimosas kwa jumla ya mabao 2-0 ikitoka suluhu ugenini na kushinda 2-0 nyumbani.

Katika mchezo huo wa fainali Yanga sc itaanzia nyumbani katika uwanja wa Benjamin Mkapa Mei 28 na marudiano yatafanyika nchini Algeria Juni 3 ambapo matokeo ya jumla ndio yatampoa mshindi kombe pamoja na medali za ubingwa ambazo zitakabidhiwa katika mchezo wa pili nchini Algeria.

banner

Bingwa wa fainali hizo anatarajiwa kupata takribani shilingi bilioni 4.7 za kitanzania huku mshindi wa pili akipata shilingi bilioni 1.9.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited