Home Makala Yanga sc Wazindua Kadi za Kielektroniki

Yanga sc Wazindua Kadi za Kielektroniki

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imezindua rasmi zoezi la ugawaji wa kadi za elektroniki za mashabiki na wanachama wa klabu hiyo leo jijini Dodoma katika hafla iliyofanyika Morena Hoteli huku mgeni rasmi akiwa spika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Tulia Akson.

Katika hafla hiyo wabunge ambao ni mashabiki na wanachama wa klabu hiyo walipatiwa kadi hizo huku wanachama na mashabiki wa kawaida wakitakiwa kukamilisha usajili kupitia matawi yao ili waweze kuzipata kadi hizo.

Kadi hizo zina faida mbalimbali ikiwemo kufanyia manunuzi mengine pamoja na kukatia tiketi ya kuingia uwanjani huku ikiwa inatengenezwa na kampuni ya N-Card.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited