Home Makala Yanga Sc Yamalizana na Chikola

Yanga Sc Yamalizana na Chikola

Yanga Sc imekamilisha usajili wa winga wa Tabora United Offen Chikola

by Sports Leo
0 comments
Yanga Sc imekamilisha usajili wa winga wa Tabora United Offen Chikola - sportslwo.co.tz

Klabu ya Yanga Sc imekamilisha usajili wa winga wa Tabora United Offen Chikola kuelekea msimu ujao wa ligi kuu na michuano ya Kimataifa 2024-2025.

Baada ya majadiliano ya pande mbili Yanga Sc wamemalizia vitu kadhaa na Tabora United Fc ambapo tayari Offen Chikola amesaini mkataba wa kuitumikia klabu hiyo.

Kiwango bora alichoonyesha  msimu huu uliomalizika kimewafanya mabosi wa yanga kukaa chini na kumaliza dili la winga huyo mapema wakiwawahi Simba Sc na Azam Fc ambao walikua wanamvizia.

banner

Kiungo huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi za winga wa kulia na kushoto pamoja na nafasi zote za ushambuliaji msimu huu alifunga mabao saba na kutoa pasi saba za mabao katika klabu hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited