Msafara wa klabu ya Yanga sc umewasili salama mkoani Singida kuelekea mchezo wa kirafiki dhidi ya Singida Black Stars siku ya kesho jumatatu machi 24.
Yanga sc inatarajiwa kumemyana na klabu hiyo ikiwa ni sehemu ya sherehe za kufungua uwanja mpya wa klabu ya Singida Black Stars unaoitwa Airtel stadium.
Katika msafara huo mastaa wa Yanga Sc ambao hawajaitwa timu za taifa wamesafiri na Timu akiwemo Stephan Aziz Ki,Bakari Mwamnyeto na Pacome Zouzoua.
Wengine ni Kibwana Shomari,Nickson Kibabage,Shadrack Boka,Maxi Nzengeli,Prince Dube sambamba na AbouTwalib Mshery,Abubakar Salum na Aboubakari Khomeini.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Mchezo unatarajiwa kuvutia mashabiki wengi mkoani humo kutokana na vikosi vya timu zote kujaa mastaa wa maana.
Mara ya mwisho timu hizo kukutana Yanga sc iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam.