Home Makala Yanga sc Yawasili Singida

Yanga sc Yawasili Singida

by Sports Leo
0 comments

Msafara wa klabu ya Yanga sc umewasili salama mkoani Singida kuelekea mchezo wa kirafiki dhidi ya Singida Black Stars siku ya kesho jumatatu machi 24.

Yanga sc inatarajiwa kumemyana na klabu hiyo ikiwa ni sehemu ya sherehe za kufungua uwanja mpya wa klabu ya Singida Black Stars unaoitwa Airtel stadium.

banner

Katika msafara huo mastaa wa Yanga Sc ambao hawajaitwa timu za taifa wamesafiri na Timu akiwemo Stephan Aziz Ki,Bakari Mwamnyeto na Pacome Zouzoua.

Wengine ni Kibwana Shomari,Nickson Kibabage,Shadrack Boka,Maxi Nzengeli,Prince Dube sambamba na AbouTwalib Mshery,Abubakar Salum na Aboubakari Khomeini.

Mchezo unatarajiwa kuvutia mashabiki wengi mkoani humo kutokana na vikosi vya timu zote kujaa mastaa wa maana.

Mara ya mwisho timu hizo kukutana Yanga sc iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited