Yanga Sc wamekanusha taarifa za mtandaoni zilizoenea kuwa wamelifuta jina la mchezaji wao wa 28,Benard Morrison kwenye orodha ya wachezaji wa msimu wa 2020/2021.
TFF iliamua kesi hiyo kwa kuliondoa jina la Morrison kwenye orodha ya wachezaji wa Yanga Sc na kulibakisha Simba Sc jambo ambalo limewafanya Yanga kutoridhika na maamuzi yao na kwenda mbele zaidi (FIFA) ili kusaka haki kwa ajili ya mchezaji huyo wanayedai kuwa bado ni mali yao.
Kaimu katibu mkuu wa Yanga Sc,Simon Patrick amesema kuwa wameshamuwekea pingamizi Morrison ambaye anaonekana kwenye orodha ya wachezaji wa Simba sc wakati bado ni mchezaji wao na yupo katika orodha ya kikosi cha msimu wa 2020/2021 .
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.