Home Riadha Tanzania Yaburuza Mkia Riadha

Tanzania Yaburuza Mkia Riadha

by Sports Leo
0 comments

Timu ya riadha kutoka Tanzania imefanya vibaya katika mashindano ya riadha Afrika yanayoendelea nchini Morocco baada ya wanariadha watatu kushika nafasi ya mwisho katika mashindano hayo.

Wanariadha hao  Ally Gulami, Benjamin Kulwa na Regina Mpigachai wameshindwa kutamba katika mbio hizo baada ya Ally Gulami kutumia sekunde 48.96 na Benjamini kula kutumia sekende 50.85 katika mbio za mita 400 huku Regina Mpigachai akitumia sekunde 2.13 mita 800.

Matokeo hayo ni pigo kwa Timu za Tanzania katika michezo hiyo ya 12, inayofanyika jijjni Rabat baada ya Judo kuondoshwa katika hatua za awali ikiwa ni siku 1 tu kabla ya hafla ya ufunguzi Agosti 19.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited