Kama kuna anaedhani Yanga inauchukulia poa mchezo dhidi ya watani zao Simba ambao utapigwa Jumapili, pole yake kwani mabingwa hao wa kihistoria wamejipanga kwelikweli kushinda mchezo huo.
Wadhamini wa klabu ya Yanga kampuni ya GSM wameahidi kutoa kitita cha Tsh Milioni 200 kama Yanga itashinda mchezo huo.
Afisa Mhamasishaji wa Yanga Antonio Nugaz amesema fedha hizo watakabidhiwa ‘taslim’ baada ya mchezo ingawa utaratibu wa makabidhiano utabadilika kutokana na wingi wake.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Aidha Nugaz amesema kuwa bado GSM wanaendeleza utaratibu wa kutoa bonas ya Tsh Milioni 10 kwa wachezaji pale timu inaposhinda ingawa kwa sasa hawatangazi.