Home Soka 200ml Kuwamaliza Simba sc

200ml Kuwamaliza Simba sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Kama kuna anaedhani Yanga inauchukulia poa mchezo dhidi ya watani zao Simba ambao utapigwa Jumapili, pole yake kwani mabingwa hao wa kihistoria wamejipanga kwelikweli kushinda mchezo huo.

Wadhamini wa klabu ya Yanga kampuni ya GSM wameahidi kutoa kitita cha Tsh Milioni 200 kama Yanga itashinda mchezo huo.

Afisa Mhamasishaji wa Yanga Antonio Nugaz amesema fedha hizo watakabidhiwa ‘taslim’ baada ya mchezo ingawa utaratibu wa makabidhiano utabadilika kutokana na wingi wake.

banner

Aidha Nugaz amesema kuwa bado GSM wanaendeleza utaratibu wa kutoa bonas ya Tsh Milioni 10 kwa wachezaji pale timu inaposhinda ingawa kwa sasa hawatangazi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited