Wachezaji wa klabu ya Atletico Madrid wamekubali kukatwa asilimia 70 ya mishahara yao huku kocha wao Diego Simeone mshahara wake utapunguzwa kwa kiasi cha Pauni Milioni 22.6 kutoka 32.6 .
Dhumuni ni kusaidia wale wafanyakazi wengine wa klabu ili kuweza kukabiliana na janga la uchumi . Kuna takribani ya wafanyakazi 430 ndani ya Atletico Madrid ambao wanafanya kazi nyuma ya pazia ambao hawaonekani uwanjani au kwenye benchi.