Home Soka Azam Fc yanasa mtambo wa mabao

Azam Fc yanasa mtambo wa mabao

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Azam imekamilisha usajili wa mshambuliaji hatari toka klabu ya Zanaco ya Zambia Rodgers Kola kwa mkataba wa miaka miwili hadi 2023.

Mzambia huyo aliifungia Zanaco fc magoli 12 katika ligi kuu ya zambia akiwa nyuma ya mshambuliaje mwenzake Zanaco Moses Phiri aliyeifunga magoli 17. mchezaji huyo pia alikuwa akihusishwa na vilabu kadhaa vya Afrika Kusini kabla ya kutua kwa matajiri hao wa jiji la Dar es salaam.

Usajili huo ni muendelezo wa Azam fc kujijenga zaidi ili kushindani na vilabu vikubwa vya Simba na Yanga pamoja na michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika baada ya ule wa awali wa kiungo mwengine Mzambia Charles Zulu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited