Taarifa kutoka Hispania zinasema Rais wa klabu ya Barcelona, Joan Laporta ana mpango wa kuwakutanisha Cristiano Ronaldo na Lionel Messi msimu ujao na yuko tayari kutoa ofa ya wachezaji wawili katika juhudi za kuishawishi Juventus kumuuza mshambuliaji huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 36.
Ronaldo amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake na Juventus na amekuwa akihusishwa na kuondoka kunako miamba hao wa Turin huku Manchester United, Real Madrid na Paris Saint-Germain zikimuhitaji lakini Barcelona wako tayari kufanya uhamisho wa kihistoria.