Klabu ya Kagera Sugar imempa mkono wa kwaheri kocha mkuu wa klabu hiyo Mecky Mexime baada ya jana kufungwa bao 1-0 na Namungo Fc katika mchezo wa ligi kuu nchini.
Mexime amekua na mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha hali iliyowalazimu mabosi wa klabu hiyo kuamua kukaa meza moja na beki huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar na timu ya taifa ya Tanzania.
“Ni kweli kama ulivyosikia, tangu jana Ijumaa jioni niliongea na viongozi na leo tumeachana, kikubwa ni matokeo ila kama kina timu ije tufanye kazi” amesema Maxime.