Home Soka CAF Yamtema Drogba

CAF Yamtema Drogba

by Sports Leo
0 comments

Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinadai kuwa shirikisho la kabumbu barani Afrika “CAF” limemfuta kazi aliyewahi kuwa mshambuliaji wa Chelsea Didier Droga kutokana na kushindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari za michezo nguli Afrika Mamadou Gaye, CAF wametengua uteuzi wa Didier Drogba kama mshauri wa Rais wa CAF Ahmad Ahmad.

Ikumbukwe kuwa July 2019 staa huyo (Drogba) na staa wa zamani wa Barcelona na Cameroon Samwel Eto’o waliteuliwa kuwa washauri wa Ahmad Ahmad lakini Drogba hajatoa mchango wowote katika kazi hiyo na wala hajawahi hudhuri shughuli yoyote ya CAF ikiwemo mechi hata moja ya AFCON 2019 toka alipoteuliwa katika ngazi hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited