Home Soka Camavinga aingia rada za Man Utd

Camavinga aingia rada za Man Utd

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji kinda wa Kifaransa Eduardo Camavinga yupo katika mipango ya kutakiwa na mashetani wekundu Manchester united katika dirisha hili la majira ya joto pindi tu itakapokamilisha dili la Jadon Sancho.

Camavinga mwenye umri wa miaka 18 anayekipiga katika klabu ya Rennes ya Ufaransa anatajwa kuwa mrithi wa Mfaransa mwenzake Paul Pogba anayehusishwa kutakiwa na matajiri PSG ya Ufaransa. Mkataba wa Pogba unatarajiwa kumalizika mwaka 2022, hivyo Man Utd wanahisi huenda wakampoteza baada ya kusuasua kwa mazungumzo ya mkataba mpya.

Man Utd itakabiliwa na upinzani kutoka katika klabu za PSG, Real Madrid na Arsenal katika kuwania saini ya kiungo huyo mahiri.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited