Home Soka Cecafa Wanawake Yanoga

Cecafa Wanawake Yanoga

by Sports Leo
0 comments

Timu mbalimbali zimeanza kuwasili Tanzania kuelekea kwenye mashindano ya Cecafa kwa Wanawake yatakayoanza Novemba 16-25,2019 Dar es Salaam.

Tayari timu za Burundi na Djibout zimetua jana Jumanne na kuelekea kwenye Hoteli zilizopangiwa.

Leo timu za Kenya na Ethiopia zinataraji kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Uganda wenyewe wanatarajia kuingia Kesho mchana sawa na Zanzibar huku pia tukiitarajia timu ya Sudan Kusini.

Wenyeji Tanzania Bara “Kilimanjaro Queens” mabingwa watetezi tayari wapo Kambini wakiendelea kujifua.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited