Home Soka Dube nje wiki sita

Dube nje wiki sita

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Azam fc Prince Dube anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda wa takribani wiki siku sita kutokana na kulazimika kufanyiwa operesheni ya maumivu anayoyasikia.

Dube amekuwa akisumbuliwa na maumivu chini ya tumbo tangu nusu fainali ya mchezo wa shirikisho dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora,baada ya kuumia alipelekwa Afrika Kusini kwa dokta Nicolas ambaye amekuwa akiwatibia wachezaji wa Azam fc,baada ya vipimo Dokta huyo alishauri achomwe sindano tu bila upasuaji.

Lakini mfumania nyavu huyo amekuwa akiendelea na maumivu kabla ya kuanguka na kushindwa kuendelea na mchezo wa kirafiki dhidi ya Kabwe Worriors ambao alifunga,na ndipo aliporudishwa tena bondeni ambapo safari hii dokta Nicolaus ameshauri afanyiwe upasuaji.

banner

Dube atakosa michezo ya awali ya mtoano kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya Horseed pamoja na michezo ya mwanzo ya ligi kuu soka Tanzania Bara.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited