Hery Sasii ni miongoni mwa waamuzi 17 walioteuliwa kuvaa beji za Shirikisho la Soka la kimataifa (FIFA) mwakani.
Taarifa ya waamuzi hao imetolewa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) na kuwataja wengine kwa waamuzi wa kati kuwa ni Florentina Zablon, Jonesia Rukyaa, Martin Saanya, Mfaume Nassoro na Ramadhan Kayoko.
Waamuzi wasaidizi ni Abdulaziz Ally, Ferdinand Chacha, Frank Komba, Hellen Mduma, Janet Balama, Kassim Mpanga, Mbaraka Haule, Mohamed Mkono na Soud Lila.
Siku za karibuni mwamuzi Henry Sasi amekua na maamuzi tata katika michezo aliyochezesha kiasi cha kuwatia hofu mashabiki kuhusu kiwango cha mwamuzi huyo hasa baada ya kuipa Simba sc penati ambayo haikua sahihi katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Kmc.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Credit:Dominick Salamba