Home Soka Gsm Kumwaga Mamilioni Yanga sc

Gsm Kumwaga Mamilioni Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Unaambiwa tajiri wa klabu ya Yanga sc Gharib Said Mohamed anajiandaa kumwaga mamilioni ya pesa kama zawadi endapo timu hiyo itatwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara baada ya kuukosa kwa miaka karibuni mitano sasa.

Iko hivi baada ya kutwaa kombe la mapinduzi bilionea huyo alitoa zawadi ya milioni mia tatu kwa wachezaji ambapo sasa katika duru la pili la ligi kuu nchini amewaahidi zawadi nono endapo watatwaa ubingwa huku wakipandishiwa bonasi za mechi wanayoshinda mpaka milioni sabini za kitanzania.

Chanzo cha ndani ya klabu hiyo kimesema uwepo wa mamilioni hayo kumemfanya kocha kaze pamoja na benchi la ufundi na wachezaji wapambane kuhakikisha wanapata matokeo kila kukicha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited