Home Soka Gsm Wainogesha Yanga

Gsm Wainogesha Yanga

by Sports Leo
0 comments

Kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Coastal union wachezaji wa Yanga wamepata zawadi wa shilingi milioni kumi kutoka kwa wadhamini na wasambazaji wa jezi za timu hiyo kampuni ya Gsm fedha ambazo zitatolewa katika kila mechi ambayo watashinda.

Gsm inayomilikiwa na tajiri Gharib Said Mohamed ambayo imedhamini Yanga kupitia godoro la Gsm Foam na huku wakilamba dili la usambazaji wa jezi za klabu hiyo kupitia maduka mbalimbali(Malls) yanayomilikiwa na kampuni hiyo imeamua kujitolea kiasi hicho cha fedha katika kila mechi ambayo timu hiyo itashinda na ambapo tayari kiasi hicho cha fedha kimekabidhiwa kwa wachezaji kufuatia ushindi huo.

Juma Abdul ambaye alikua nahodha kwenye mchezo huo kufuatia kutokuwepo kwa nahodha mkuu Papy Kabamba Tshitshimbi ambaye anasumbuliwa na majeraha tayari amethibitisha wachezaji kupokea kiasi hicho cha fedha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited