Makamu Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Yanga sc Eng.Hersi Said ameingilia kati suala la kocha wa Yanga princess Edna Lema ambaye aliamua kuachana na klabu hiyo baada ya msimu wa ligi ya wanawake kuisha.
Kocha huyo amefanya mazungumzo ya ana kwa ana na Injinia Hersi Saidi ambaye ame share mazungumzo hayo kupitia Live ya mtandao wa Instagram na hatimaye mazungumzo hayo kuisha kwa makubaliano ya pande zote mbili.
Inadaiwa kocha huyo amekubali kurejea klabuni hapo baada ya kukubaliana dau la usajili na injinia ambapo kocha huyo atapewa stahiki zake anazotaka ili kusalia jangwani.