Home Soka Juventus Watwaa Ubingwa Serie A

Juventus Watwaa Ubingwa Serie A

by Sports Leo
0 comments

 

Rasmi Juventus ni mabingwa wa Italia wakiwa na mechi mbili mkononi baada ya kuibuka na ushindinwa mabao 2-0 dhidi ya Sampdoria na kufanikiwa kucheza mechi 36 kati ya 38 na kufikisha alama 83 ambazo hazitafikiwa na timu nyingine.

Mabao ya bibi kizee hao yalifungwa na Cristiano Ronaldo pamoja na Bernadeschi na kuwaacha wapinzani wao wanaoshika nafasi ya Pili Inter Milan wenye alama zao 76.

banner

Ronaldo amefikisha goli lake la 31 msimu huu katika ligi nyuma ya kinara Ciro Immobile anayeichezea Lazio Fc mwenye magoli 34.

Juventus wanatwaa ubingwa huo kwa mara ya tisa mfululizo huku usajili wao wa mastaa kama Ronaldo ukionekana kuwalipa zaidi japo wana umri mkubwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited