Home Soka Kagere Agomea Dili La Ulaya

Kagere Agomea Dili La Ulaya

by Sports Leo
0 comments

Kwa mujibu wa meneja wa mchezaji wa klabu ya Simba Meddie Kagere aitwaye Patrick Gakumba ni kwamba mshambuliaji huyo amegomea ofa ya kujiunga na klabu ya Levante Fc ya nchini Hispania.

Meneja huyo raia wa Rwanda alibainisha kwamba klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu nchini Hispania maarufu kama La liga ilimuona Kagere wakati akiitumikia klabu ya Simba katika mchezo dhidi ya klabu ya Sevilla ambapo walionyesha nia ya kumsajili japokua mkataba aliokua nao na Simba sc ndio ulikua kikwazo.

Gakumba amebainisha kwamba hivi sasa staa huyi tayari anahitajika na timu hiyo japokua hawajakubaliana na suala la kufanya majaribio ya miezi sita kama wanavyotaka wahispania hao.

banner

Hata hivyo inasemekana staa huyo mzaliwa wa Burundi mwenye uraia wa Rwanda tayari amekubaliana dau na klabu yake ya Simba na ataongeza mkataba.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited