Home Soka Kagere Mbioni Kutimka Simba sc

Kagere Mbioni Kutimka Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Wakala wa mshambuliaji wa Simba sc Meddie Kagere amethibitisha kumtafutia timu mshambuliaji huyo nchini Marekani ambapo anaweza kujiunga na timu hiyo msimu ujao endapo atafakisha mabao 25 ya ligi kuu na michuano mengine ambayo Simba sc inashiriki.

Wakala huyo Patrick Gakumba amesema tayari mchezaji tayari ana ofa kutoka Dallas Fc inayoshiriki ligi kuu nchini Marekani maarufu kama Major Soccer League ambapo moja ya masharti aliyopewa na timu hiyo ni kuhakikisha anafunga idadi hiyo ya magoli kwa msimu huu.

Kagere alijiunga na Simba sc akitokea Gormahia ya nchini Kenya ambapo toka ajiunge na timu hiyo amekua akifanya vizuri kiasi cha kuchukua tuzo mbalimbali ikiwemo ufungaji bora wa ligi kuu msimu uliopita.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited