Home Soka Kapombe Asaini Miwili Simba

Kapombe Asaini Miwili Simba

by Sports Leo
0 comments

Beki wa Simba sc Shomari Kapombe amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kusalia klabuni hapo baada ya mkataba wa awali wa miaka miwili kumalizika mwezi huu.

Beki huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi zote za idara ya ulinzi pamoja na kiungo amesaini mkataba mpya licha ya kutokuwa na misimu mizuri tangu ajiunge klabuni hapo ambapo amekua akisumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara tangu ajiunge akitokea Azam Fc ambapo nako hakuwa na msimu mzuri baada ya kuugua kwa muda na kutibiwa nchini Afrika ya kusini.

banner

Hivi karibuni beki huyo alizua sintofahamu baada ya taarifa kudai amejitonesha majeraha akiwa katika kambi ya timu ya taifa inayojiandaa na michuano ya Afcon japo mwenyewe alikanusha na kusema hajajiunga na timu hiyo kwa kuwa hajapona vizuri na ana programu maalumu ya matibabu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited