Home Soka Kibu,Kibwana waongezwa Stars

Kibu,Kibwana waongezwa Stars

by Sports Leo
0 comments

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa miguu ‘Taifa Stars’ Kim Poulsen amewaongeza kikosini mshambuliaji wa Simba Sc Kibu Denis na beki wa Yanga Sc Kibwana Shomari katika kikosi hicho.

Kim alionesha kumhitaji sana Kibu Denis kiasi cha kupelekea TFF kumuombea uraia mchezaji huyo kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambapo alipewa uraia wa Tanzania Septemba 30.

banner

Kwa upande wa Kibwana ambaye amekuwa katika kiwango kizuri tangu ajiunge na Yanga msimu uliopita hatimaye amepata nafasi aliyostahili mara baada ya wadau wa soka nchini kuhoji kwanini hajumuishwi ndani ya kikosi hicho,na huenda akawa mbadala wa Shomari Kapombe ambae alipata majeraha kidogo kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Biashara United.

Taifa Stars itakabiliana na Benin siku ya Alhamisi katika mchezo wa tatu wa kufuzu kombe la dunia Qatar 2022 kabla ya kurudiana nao tena Oktoba 10 ugenini,wakati huo huo kiungo Jonas Mkude ameomba kuondolewa kwenye kikosi hicho kutokana na sababu za kifamilia na ameruhusiwa na kocha Kim.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited