Home Soka Kmc Warejea Dar

Kmc Warejea Dar

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha KMC FC kimerejea jijini Dar es Salaam leo kikitokea mkoani Tanga ikiwa ni baada ya kumalizika kwa mchezo wa jana dhidi ya Coast Union uliopigwa katika uwanja wa Mkwakwani na kumalizika kwa sare ya kutokufungana.

KMC FC imerejea Jijini Dar es Salaam ambapo kesho itaendelea na mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo mwingine wa Ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Ruvu Shooting mchezo utakao chezwa katika uwanja wa Uhuru saa 16: 00 mchana.

KMC FC iliondoka Jijini Dar es Salaa, Machi mbili ambapo iliwasili Jijini Arusha na kucheza mchezo wake wa Ligi Kuu Machi Nne katika uwanja wa Sheih Amri Abeid dhidi ya Polisi Tanzania mchezo uliomalizika kwa Kino Boys kupoteza kwa kufungwa goli moja kwa bila.

Nb:Imetolewa na Afisa Habari Wa Kmc Fc Christina Mwagala

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited