Home Soka Kocha Simba Aipa Tano Gsm

Kocha Simba Aipa Tano Gsm

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa klabu ya Simba sc Jamhuri Kihwelu “Julio” ameipongeza kampuni ya Gsm baada ya kukubali kuendelea kuisaidia klabu ya Yanga baada ya kuandika barua ya kusitisha mambo yote yaliyopo nje ya mkataba.

Julio amesema licha ya kampuni hiyo ina malengo yake ya kibiashara, ila inachokifanya kuisaidia timu hiyo nje na mkataba ni zaidi ya mapenzi ambayo yanapaswa kuungwa mkono ili kuifanya timu iendelee kuwa na ufanisi na kuipa thamani yake timu hiyo.

“GSM ni mfanyabiashara anafanya vitu kwa faida, lakini kwa mapenzi yake aliamua kuwasaidia zaidi ya mkataba wake na alichowekeza na unajua Yanga ilikuwa na changamoto nyingi kuanzia usajili, mishahara na mengineyo ya ziada wanapaswa kuungwa mkono na sio kuwabughudhi,” Alisema Kocha huyo aliyewahi kuifundisha klabu ya Simba sc mara kadhaa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited