Home Soka Luvanga Akutana na Ronaldo

Luvanga Akutana na Ronaldo

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji wa Al Nassr ya Saudia,Mtanzania Clara Luvanga wa timu ya wanawake amekutana ana kwa ana na mshambuliaji wa klabu hiyo kwa upande wa wanaume Cristiano Ronaldo na kufanikiwa kupiga picha ya pamoja ambayo imesambaa katika mitandao ya kijamii hapa nchini.

Clara mchezaji wa zamani wa Yanga Princess alijiunga na klabu hiyo msimu huu akitokea klabu ya Dux Logrono ya nchini Hispania na baada ya takribani miezi mitatu alijiunga na klabu ya Al Nassr ambayo ilivunja mkataba wake na kumnunu moja kwa moja na amefanikiwa kupatia timu hiyo ubingwa wa ligi kuu ya wanawake nchini humo.

Mpaka sasa haijafahamika kama picha hiyo ilipigwa wakati kukiwa na tukio maalumu ama lakini ni jambo rahisi kwao kuonana kwa kuwa wote wanatumikia klabu moja japo wapo timu mbili tofauti zinazomilikiwa na mmiliki mmoja.

banner

Mshambuliaji huyo tangu ajiunge na timu hiyo ya wanawake mwaka jana mwezi oktoba amefunga jumla ya mabao 10 katika michezo tisa ya ligi kuu nchini humo na ameisaidia timu hiyo kutwaa kombe la ligi kuu ya wanawake nchini humo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited