Home Soka Manula Ampa Tano Morrison

Manula Ampa Tano Morrison

by Sports Leo
0 comments

Kipa namba moja wa timu ya Taifa ya Tanzania na klabu ya Simba Aishi Manula amempongeza staa wa klabu ya Yanga Benard Morrison baada ya kumfunga bao katika mechi baina ya watani wa jadi Yanga dhidi ya Simba.

Katika mchezo huo dakika ya 44 Morrison alipiga faulo iliyoenda moja kwa moja langoni na kumuacha kipa huyo akiwa anashangaa kutokana na kasi na ufundi uliotumika kupiga mpira huo.

Akihojiwa na kituo kimoja cha radio nchini Kipa huyo alimpongeza mpigaji baada ya kutumia akili kupiga mpira huo uliokua na kasi huku ukifanikiwa kuwapita mabeki wa klabu hiyo.

banner

Bao hilo liliwafanya Yanga kupata ushindi wa kwanza baada ya miaka minne katika pambano la watani wa jadi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited