Home Soka Manula Basi Tena Simba Sc

Manula Basi Tena Simba Sc

by Sports Leo
0 comments

Golikipa wa Simba sc na Timu ya Taifa ya Tanzania Aishi Manula ataikosa michezo miwili ya robo fainali ya Klabu yake ya Simba dhidi ya Al Ahly kutokana na kupata majeraha akiwa na Timu ya Taifa ilipokua ikicheza na Bulgaria nchini Azerbaijan.

Manula aliumia kipindi cha kwanza katika mchezo huo na taarifa zinaeleza kuwa Manula ametonesha jeraha lake ambalo alilipata kipindi cha nyuma hali iliyopelekea kufanya upasuaji ambao ulimlazimu kukaa nje Kwa miezi kadhaa.

Kwa mujibu wa meneja wa mchezaji huyo Jemedari Said  amesema kuwa jeraha hilo litamfanya sasa kukaa nje ya Uwanja Kwa muda mrefu zaidi ili kuhakikisha anapona kabisa na kukaa sawa ndipo anaweza kuanza tena kucheza mechi za ushindani.

banner

Simba sc siku ya Jumamosi ijumaa itakua na mchezo mgumu dhidi ya Al Ahly ambapo sasa ni wazi golini atakaa kipa Ayoub Lakred huku Ally Salim atakaa kama kipa wa akiba ambapo pia anaweza kukaa kipa Hussein Abel.

Manula tangu arejeaa kutoka katika majeraha hayo hajaweza kurudisha kiwango chake cha awali ambapo amekua akifunga mabao rahisi tofauti na awali ikiwemo kipigo cha 5-1 kutoka kwa Yanga sc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited