Home Soka Manula- Sina Tatizo na Ndayiragije

Manula- Sina Tatizo na Ndayiragije

by Sports Leo
0 comments

Imeelezwa kuwa kipa wa klabu ya Simba, Aishi Manula amesema anaheshimu maamuzi ya kocha Mrundi, Ettiene Ndayiragije kutomuita katika kikosi cha Taifa Stars.

Siku kadhaa zilizopita Ndayiragije alitangaza kikosi cha Stars ambacho kitacheza mechi za kuwania kufuzu AFCON dhidi ya Libya na Equatorial Guinea.

Manula ameeleza kuwa kutoitwa kwake wala haiwezi kumkatisha tamaa kwani ni maamuzi ya kocha na anachukulia jambo la kawaida.

banner

Kipa huyo ameongeza kuwa kwa sasa yupo fiti asilimia 100 na anawatakia kila la kheri wachezaji wenzake ambao wameitwa kwa ajili ya mechi hizo mbili.

Manula amekuwa hana bahati ya kuwa sehemu ya kikosi hicho tangu aitwe mara moja wakati Stars ikiwa na kibarua cha kufuzu CHAN dhidi ya Kenya.

Habari hii kwa msaada wa Salehe Jembe blog.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited