Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania(TFF) limetangaza kuwa kuanzia msimu ujao wa ligi kuu soka Bara idadi ya wachezaji wa kigeni watakaoruhusiwa kusajili kwenye vilabu shiriki ni 12.
Mabadiliko hayo yametangazwa hii leo na sasa kuanzia msimu ujao idadi ya wachezaji wa kigeni watakaoruhusiwa kuanza katika mchezo wa ligi kuu itakuwa ni 8 khu watano wakianzia benchi.
Idadi hiyo itaenda kuzinufaisha moja kwa moja timu za Simba,Yanga na Azam hasa katika mashindano ya kimataifa ukizingatia wapo katika harakati za usajili kuziimarisha timu zao.