Home Soka Mexime Akubali Mziki wa Simba sc

Mexime Akubali Mziki wa Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Kagera Sugar Mecky Mexime ameukubali uwezo wa kikosi cha Simba baada ya kufungwa mabao 3-0 katika uwanja wa nyumbani wa Kaitaba uliopo mjini Bukoba mkoani Kagera mchezo uliofanyika jana.

Awali kocha  huyo alijitapa atawafunga Simba sc akiringia rekodi yake ya msimu uliopita alopowafunga wanamsimbazi hao mechi zote za nyumbani na ugenini.

Tambo hizo zilikoma baada ya dakika 90 za mchezo huo kufuatia mabao ya Meddie Kagere aliyefunga mawili na Mohamed Hussein yaliyoipa pointi tatu simba ugenini.

banner

“Simba ni timu bora sio tu ndani ya nchi bali hata Afrika ukitaja timu bora nne simba itakuwemo,lSisi tulifanya makosa kadhaa na wenzetu wameyatumia”.Alisema Mexime

Kagera ilikua imeshinda mechi zote za awali na kuwafanya kuongoza ligi kwa kuwa na pointi tisa kabla ya jana kukubali kipigo hicho.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited