Home Soka Moloko Atua Libya

Moloko Atua Libya

by Sports Leo
0 comments

Siku chache baada ya kuachana na klabu ya Yanga sc winga Jesus Moloko ameamua kujiunga na klabu ya Al Sadaqa SC Benghazi inayoshiriki Ligi Kuu ya Libya akiungana na aliyekua mshambuliaji wa Simba Sc Jean Baleke kukipiga nchini humo.

Kusajiliwa kwa Moloko nchini humo kumehitimisha tetesi za klabu za hapa nchini zilizokua na mpango wa kumsajili mshambuliaji huyo ikiwemo Geita Gold Fc ambayo ilikua mstari wa mbele kuhakikisha inamsajili staa huyo wakati wa dirisha dogo la usajili.

Winga huyo sasa atakipiga ligi moja na aliyekuwa mshambuliji wa mshambuliaji wa Simba Jean Baleke ambaye amesajiliwa ya Al Ittihad baada ya TP Mazembe kumtoa tena kwa mkopo na alimalizana na Simba baada ya muda wake wa mkopo kumalizika sasa atakuwa akikiwasha katika klabu hiyo, hadi Januari 30, 2025.

banner

“Muda mchache kabla ya dirisha la usajili kufungwa winga Mkongomani Jesus Moloko atakuwa sehemu ya ngome yetu akitoka Yanga ya Tanzania”Ilisomeka taarifa ya klabu hiyo ambayo ipo nafasi ya nane ya msimamo wa ligi kuu nchini humo ikiwa na alama sita baada ya kucheza michezo tisa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited