Home Soka Morrison Arejea Yanga

Morrison Arejea Yanga

by Dennis Msotwa
0 comments

Habari njema ni kuwa kiungo mshambuliaji Bernard Morrison anaweza kurejea baada ya hali yake kuimarika kwa haraka baada ya kupata majeraha ya mguu.

Morrison alipata majeraha kabla ya mchezo dhidi ya Simba ambao alicheza kwa dakika 56 kabla ya kutolewa kumpisha Patrick Sibomana huku akiwa amefunga bao moja na ushindi kwa njia ya faulo.

Mchezo dhidi ya Namungo unatarajiwa kuwa na upinzani mkali kutokana na ukweli kuwa Namungo ni moja ya timu bora msimu huu.

Ni mchezo ambao Yanga inahitaji matokeo ya ushindi hasa baada ya kupoteza mchezo uliopita ili kuwania nafasi ya pili ya ligi kuu kutengeneza mazingira mazuri ya kucheza michuano ya kimataifa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited