Home Soka Morrison Atupwa Kakaangoni

Morrison Atupwa Kakaangoni

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji wa Yanga SC Bernard Morrison amepelekwa Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kosa la kumpiga kiwiko mchezaji wa Tanzania Prisons FC Jeremia Juma wakati mpira ukiwa umesimama kwenye mchezo uliofanyika Februari 15, 2020 uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na shirikisho la soka nchini(Tff) imesema mchezaji huyo amepelekwa kwenye kamati hiyo ambayo itakaa na kutoa hukumu kwa mujibu wa sheria.

Suala la mchezaji huyo limekua na kelele nyingi hasa ikizingatiwa mechi baina ya watani wa jadi Simba na Yanga ikiwa imekaribia huku wale wa Yanga wakihisi kufanyiwa hujuma ili mchezaji huyo aikose mechi hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited