Home Soka Morrison Mpaka Kesho

Morrison Mpaka Kesho

by Sports Leo
0 comments

Ile kesi iliyoshika nyoyo za wapenzi wa soka nchini hasa wa klabu za Simba sc na Yanga sc kuhusu usajili wa mchezaji Benard Morrison itaendelea tena kesho baada ya leo kushindwa kutolewa maamuzi licha ya pande zote mbili kusikilizwa.

Awali taarifa zilidai kuwa mchezaji huyo ni mali ya Yanga sc baada ya tetesi kudai klabu hiyo imeshinda kesi hiyo lakini mpaka tunaingia mitamboni huku kikao kikiisha bila hukumu hiyo kusomwa rasmi.

Kesi hiyo ya mgogoro wa kimkataba kati ya klabu hiyo na Benard Morrisson imeteka nyoyo za wapenzi wengi wa soka hasa baada ya staa huyo kusaini klabu ya Simba sc ambayo imemtambulisha rasmi kama mchezaji wao.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited