Imeripotiwa kwamba kiasi cha mshahara anaolipwa straika Heritier Makambo na klabu ya Horoya ndio kikwazo kikuu cha kumrudisha katika klabu ya Yanga sc.
Makambo aliuzwa na Yanga kwenda Horoya ya nchini Guinnea kwa mkataba wa miaka mitatu inaelezwa yuko tayari kurudi mitaa ya Jangwani endapo timu hiyo itamhakikishia mshahara mnono kama anaolipwa na klabu hiyo.
Kwa mujibu wa kocha Mwinyi Zahera ambaye alimleta Makambo nchini amesema ni ngumu staa huyo kurejea kutokana na maslahi anayolipwa huko ambapo kwa Yanga ni ngumu kuyapata.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.