Home Soka Mzize Aikoa Yanga sc

Mzize Aikoa Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Goli la dakika ya 71 la Clement Mzize limefanikiwa kuiokoa Yanga sc na kupata alama tatu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union uliofanyika katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Yanga sc ikianza na mastaa wale wale walioiua Simba sc kwa mabao 5-1 isipokua Djigui Diarra na Joyce Lomalisa pamoja na Nahodha Bakari Mwamnyeto ilifanikiwa kuimilika Coastal ambao muda mwingi walikaa nyuma ya mpira.

Safu ya ushambuliaji ya Yanga sc ilionekana kukosa maarifa ya kuivuka safu ya ulinzi ya Coastal iliyokua chini ya Lameck Lawi ambapo Kennedy Musonda na Aziz Ki walikosa maarifa ya kuivuka safu hiyo ya ulinzi.

banner

Kipindi cha pili Kocha Miguel Gamondi aliwatambulisha mchezoni Jesus Moloko na Clement Mzize ambaye alifanikiwa kufunga kwa kichwa akimalizia krosi ya Moloko aliyepokea pasi ya Stephane Aziz Ki.

Yanga sc sasa ipo kileleni mwa msimamo wa ligi ya Nbc wakiwa na alama 24 huku Coastal Union wakisalia katika nafasi ya 13 wakiwa na alama saba katika michezo tisa ya ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited