Home Soka Ninja Amerudi

Ninja Amerudi

by Sports Leo
0 comments

Beki wa klabu ya Yanga sc Abdala Shaibu Ninja amerejea katika kikosi cha timu hiyo akitokea katika majeraha baada ya kuwa nje kwa takribani wiki tatu akitibu majeraha.

Kurejea kwa beki huyo imekuwa ni faraja kwa kikosi hicho kuelekea katika mchezo mgumu wa ligi kuu dhidi ya watani wao wa jadi Simba sc ambao utafanyika kesho mkoani Dar es salaam katika uwanja wa mkapa.

Kurejea kwa beki kunafanya klabu hiyo iwe na uhakika wa ulinzi akiungana na Bakari Mwamnyeto na Dickson Job huku Lamine Moro akiwa amesimamishwa kutokana na utovu wa nidhamu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited