Home Soka “Nitaendelea Kufungwa Tu”-Manula

“Nitaendelea Kufungwa Tu”-Manula

by Sports Leo
0 comments

Kipa wa timu ya Simba sc Aishi Manula amesisitiza kuwa ataendelea kufungwa endapo atakaa langoni kuidakia timu hiyo katika michezo mbalimbali.

Manula alibainisha hayo wakati akimjibu shabiki mmoja katika mtandao wa instagram baada ya shabiki huyo anayetumia jina la Oscarlameck3420 kumtaka kipa huyo kuwa siriazi na kazi pia apunguze makosa madogo madogo.

Ujumbe huo ulionekana kumkera kipa huyo na ndipo alipoamua kujibu kuwa ataendelea kufungwa tu.

banner

“Nitaendelea kufungwa kwa vyovyote vile iwe mbali au karibu,Iwe pembeni ama kati njia pekee ya mimi kutofungwa na kukaa benchi tu.Aliandika kipa huyo

Manula amekua na misukosuko baada ya kufungwa bao na Balama Mapinduzi katika mchezo wa watani wa jadi hali iliyosababisha awekwe benchi huku nafasi yake ikichukuliwa na Benno Kakolanya japo jana alicheza dhidi ya mtibwa na kufanya vizuri.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited