Home Soka Rasmi Ettiene,Tff Wapeana Talaka

Rasmi Ettiene,Tff Wapeana Talaka

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la mpira nchini (Tff) limeachana rasmi na kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Ettiene Ndayiragije baada ya kuamua kuvunja nae mkataba kwa makubaliano ya pande zote.

Awali taarifa zilizagaa kuhusu shirikisho hilo kuachana na kocha huyo huku ujio wa kocha Kim Poulsen ukichagiza tetesi hizo lakini taarifa rasmi iliyotolewa leo na shirikisho hilo imehitimisha suala hilo.

Ettiene ameingoza Stars katika michuano mbalimbali na kufanikiwa kuivusha mpaka katika michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani(Chan) huku akitolewa katika hatua ya makundi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited