Home Soka Samba Yatawala Simba sc

Samba Yatawala Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Katika kukiimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao wa ligi kuu Tanzania bara na michuano ya kimataifa timu ya Simba sc imemsaini mchezaji mwengine kutoka nchini Brazil na kufikisha idadi ya wachezaji watatu kutoka nchini humo.

Mchezaji huyo anayecheza nafasi ya  ulinzi anaitwa Tairone Santos Da Silva mwenye miaka 30 amesaini mkataba wa miaka miwili akitokea nchini brazil katika timu ya Atletico Cearense Fc iliyoanzishwa mwaka 1982 katika mji wa Ceara nchini humo.

Beki huyo mrefu amesajiliwa ili kuziba mapengo ya baadhi ya wachezaji akiwemo Paschal Wawa ambaye amemaliza mkataba na klabu hiyo yenye makao makuu msimbazi jijini Dar es salaam.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited