Home Soka Simba sc Yainyuka Singida Fg

Simba sc Yainyuka Singida Fg

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kuibuka na alama tatu muhimu katika mchezo dhidi ya Singida Fountain Gate uliofanyika katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salaam baada ya kuifunga tiimu hiyo mabao 3-1 na kuendelea kuipambania nafasi ya kuchukua ubingwa wa kombe la ligi kuu nchini.

Iliwachukua Simba sc dakika nane pekee kupata mabao mawili ya harakaharaka yaliyofungwa na Saido Ntibanzokiza aliyekua mwiba mchungu kwa Singida Fg katika mchezo huo ambapo alifunga bao la kwanza dakika ya sita ya mchezo baada ya mabeki wa Singida kuzembea kuokoa mpira uliozagaa ndani ya boksi la hatari kufuatia kipa Benjamini Haule kupangua shuti kali la Cletous Chama huku akifunga bao la pili kwa penati baada ya beki Laurean Makame kuunawa mpira.

Simba sc ilifanikiwa kupata bao la tatu baada ya mshambuliaji Fredy Michael kufanya kazi ya ziada kuwatoka walinzi wa klabu ya Singida Fg na kupiga shuti ambalo liligongwa na beki na kumpita kipa Benjamini Haule na kumawamaliza kabisa Singida Fg ambao hawakua na la kufanya.

banner

Saido sasa anafikisha mabao saba katika ligi kuu msimu huu huku klabu yake ya Simba sc ikifikisha alama 42 katika michezo 18 ya ligi kuu ambapo sasa wamezidiwa alama nane na vinara wa ligi kuu ya Nbc Yanga sc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited