Home Soka Simba Yang’oa Straika Tp Mazembe

Simba Yang’oa Straika Tp Mazembe

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imemvuta mshambuliaji Deo Kanda kutoka Tp mazembe ya Kongo kwa usajili wa mkopo wa msimu mmoja baada ya Pande mbili kukubaliana.

Taarifa iliyothibitishwa na Mabingwa hao mara tano barani Afrika imesema kuwa mshambuliaji huyo yupo nchini kwa lengo la kukubaliana maslahi binafsi na mabingwa hao mara mbili mfululizo wa ligi kuu ya Tanzania bara na kisha kukamilisha taratibu za usajili.

Kanda 29′ ni mchezaji mzoefu wa soka la Afrika baada ya kuzitumikia timu za Dc Motema Pembe,As vita,Raja Casablanca na pia ameichezea timu ya taifa la Kongo mechi 21 akifunga magoli manne.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited