Home Soka Stars Yamtibulia Kibarua Migne

Stars Yamtibulia Kibarua Migne

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la soka la Kenya (FKF) limesitisha ajira ya kocha wa timu hiyo mfaransa Sebastien Migne kutokana na matokeo yasiyoridhisha ya timu ya taifa (Harambee stars) katika michuano mbalimbali hivi karibuni.

Harambee stars licha ya kufanya vibaya katika michuano ya Afcon nchini Misri pia hivi karibuni ilitolewa na Taifa stars katika michezo ya awali kutafuta nafasi ya kushiriki michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) baada ya kufungwa kwa mikwaju ya penati katika mchezo wa raundi ya pili jijini Nairobi.

Katika taarifa iliyotolewa na shirikisho la nchini humo ilisomeka “Shirikisho la soka la Kenya na kocha Sebastien Migne tumekubaliana kusitisha mkataba baina yetu,hata hivyo shirikisho linamshukuru Migne kwa kufanikiwa kuwezesha kufuzu michuano ya Afcon baada ya miaka 15”.

banner

Migne ataungana na orodha ndefu ya makocha waliotimuliwa baada ya kufanya vibaya katika michuano ya Afcon akiwemo kocha wa Taifa stars Emmanuel Amunike.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited