Home Soka TPLB Yawashukia Waamuzi

TPLB Yawashukia Waamuzi

by Sports Leo
0 comments

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Februari 03, 2020 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya uamuzi ufuatao;

Mechi namba 150: Simba SC 3 v Namungo FC 2-Mwamuzi msaidizi namba mbili Kassim Safisha amefungiwa miaka mitatu(3) kwa kosa la kushindwa kutafsiri sheria ya kuotea katika mechi hiyo.

Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni namba 39(1)(a) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.

banner

Mechi namba 157: Azam FC 1 v Mtibwa FC 1-Mwamuzi Meshack Suda ameandikiwa barua ya kukumbushwa kufanya majukumu yake kwa umakini zaidi katika mechi iliyochezwa Januari 30,2020 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Vile vile katika mchezo huo Kamishina Abdallah Zongo ameondolewa kwenye orodha ya Makamishina kwa kosa la kutoa taarifa yenye mapungufu.Adhabu hii ni kwa kuzingatia Kanuni namba 40(1) kuhusu Udhibiti Kamishina

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited