Habari za ndani ya klabu ya Yanga zinadai kuwa klabu hiyo imefikia makubaliano ya mkataba wa miaka miwili na nahodha wa klabu hiyo Papy Kabamba Tshitshimbi kuendelea kukichezea klabu hiyo.
Inaelezwa mkataba wa kiungo huyo atavuna mshahara wa shilingi za kitanzania milioni nane huku dau la usajili likidaiwa kuwa ni milioni 100 za kitanzania kwa muda huo wa miaka miwili ambazo zitalipwa kwa awamu.
Mkataba wa Tshitshimbi na klabu hiyo umebakiza miezi minne uweze kufika tamati na tayari alikua akinyemelewa na Simba sc pamoja na Azam Fc huku klabu ya Tp Mazembe nayo ikitajwa kumhitaji kiungo huyo mwenye mapafu ya Mbwa.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.