Home Soka Ujenzi uwanja wa mpira Dodoma mbioni

Ujenzi uwanja wa mpira Dodoma mbioni

by Sports Leo
0 comments

Msemaji mkuu wa Serikali Mheshimiwa Gerson Msigwa amesema kuwa ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa michezo uliopangwa kujengwa makao makuu ya nchi Dodoma uko palepale na hivi karibuni utaanza kujengwa.

Ujenzi wa uwanja huo uliasisiwa na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Hayati John Pombe Magufuli likiwa ni ombi lake kwa mfalme wa Morocco Mohammed wa sita alipokuwa nchini kwa ziara maalum mwaka 2016.

Ukimya wa muda mrefu juu ya jambo hilo na wasiwasi wa Watanzania ndio umemuibua msemaji wa serikali na kusema kuwa ”dhamira ya kujenga uwanja wa mpira jijini bado ipo,serikali inakamilisha michoro ambacho mchakato huu ukikamilika,zabuni itatangazwa na ujenzi utaanza”.

banner

Msigwa pia alisema kuwa serikali imepeleka Tsh Bilioni 1.5 kwenye Baraza la Michezo la Taifa (BMT) ili kuimarisha michezo,aidha serikali imeondoa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye nyasi za bandia ili kuimarisha miundombinu ya michezo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited