Klabu za Man Utd na Real Madrid zimefika makubaliano ya kuuziana beki wa Kifaransa Rafael Varane kwa ada inayokadiriwa kufika paundi milioni 40.
Kambi ya Varane kwasasa inasubiria taratibu za covid-19 ili kuweza kuingia nchini England kwa ajili ya vipimo vya afya na kutangazwa rasmi kuwa mchezaji wa mashetani wekundu Man Utd.
Kitasa hicho kitasaini mkataba wa miaka mitano hadi mwaka 2026 kukipiga Old Trafford na anakuwa usajili wa pili kwa Man Ud baada ya ule wa Jadon Sancho.