Home Soka Waarabu Wafika Bei Kwa Morrison

Waarabu Wafika Bei Kwa Morrison

by Sports Leo
0 comments

Inaelezwa klabu moja kutoka huko Arabuni inajipanga kuleta ofa Jangwani baada ya kuvutiwa na uwezo wa winga Bernard Morrison aliyesajiliwa na klabu hiyo mwezi Januari mwaka huu

Klabu hiyo inayomilikiwa na matajiri wa mafuta, imeandaa kitita cha zaidi ya Tsh Milioni 900 kwa ajili ya kumnasa nyota huyo ambapo dau hilo ni maalumu kwa ajili ya kuvunja mkataba wa miaka miwili wa nyota huyo aliousaini msimu huu.

Taarifa tuliopata Morrison ameandaliwa mshahara wa Tsh Milioni 17 kwa mwezi pesa ambayo waarabu hao wanaamini inatosha kabisa kumshawishi winga huyo kuhama Jangwani.

banner

Taarifa kutoka ndani ya Yanga zinaelezwa kuwa klabu hiyo inasubiri barua rasmi ili kuijadili na kutoa uamuzi kuhusu kufanyika kwa biashara hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited